Search This Blog

Thursday, December 31, 2020

Tani 52 za mchele zateketezwa Zanzibar


Wakala wa Chakula na Dawa Zanzibar (ZFDA) imeteketeza tani 52 za mchele ulioingizwa nchini na Mfanyabiashara Suleiman Abdalla mwezi Machi mwaka jana ukiwa umeshaharibika na haufai kwa matumizi ya binadamu.

Mchele huo ambao ulikuwa umo kwenye makontena mawili bandarini Malindi, ulitakiwa urejeshwe ulikonunuliwa ama uangamizwe kwa gharama za mfanyabiashara mwenyewe na alikubali kugharamia zoezi la kuuangamiza.

Mkurugenzi Idara za Huduma za Maabara wa Wakala wa Chakula na Dawa Zanzibar Nadir Khatib Hassan, ambae alisimamia uangamizaji huo katika jaa la Kibele, alisema uliingizwa nchini tarehe 15.3.2019 kutoka Pakistan.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...