Baada ya mapumziko ya miezi 9 kkutokana na janga la corona, safari za ndege kutoka Dubai kwenda Istanbul zinaanza tena.
Kampuni ya Flydubai, yenye makao yake makuu huko Dubai, imetangaza kwamba ndege za Dubai-Istanbul zitaanza tena kuanzia Desemba 17 katika Uwanja wa Ndege wa Sabiha Gökçen.
Uuzaji wa tiketi umeshaanza.
Flydubai ilisitisha safari zake za Istanbul mnamo Machi 17, 2020, kama sehemu ya hatua za kupambana na Covid-19.

No comments:
Post a Comment