Search This Blog

Thursday, December 10, 2020

Rais wa zamani wa Malawi ‘apinga kuzuiwa kwa akaunti zake ‘


Rais wa zamani wa Malawi Peter Muthatika ametishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya benki ya nchini humo baada ya akaunti zake kuzuiwa na chombo cha taasisi ya kupambana na rushwa mwezi Agosti, Gazeti la the Nation nchini humo limeripoti.


Gazeti hilo limeelezea barua kutoka kwa mwanasheria wa Mutharika inayosema kuwa muda wa notisi ya zuio la akaunti zake umekwisha.


Taasisi ya kupambana na rushwa (ACB) ilizuia akaunti za Bw. Mutharika na mkewe kutokana na ‘’utoaji fedha uliokanganya’’ wakati wa uchunguzi wa ukwepaji kodi wakati wa kuingiza mifuko 800,000 ya cement.


Makosa hayo yanadaiwa kufanywa mwaka 2018 na 2019 wakati Bwana Mutharika alipokuwa madarakani.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...