Rais Dkt. Magufuli ameeleza kusikitishwa na kifo cha Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Harold Nsekela.
Dkt. Magufuli ametuma salamu za pole kwa familia na kusema Jaji Mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapakazi
"Nimesikitishwa na kifo cha Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Harold Nsekela. Poleni familia, watumishi wote wa Sekretarieti ya Maadili na Mahakama. Jaji Mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapakazi. Mungu amweke mahali pema, Amina" - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Magufuli

No comments:
Post a Comment