Waziri wa Mambo ya Ndani Süleyman Soylu, alifanya mkutano kwa njia ya video na Wazir mwenzie wa Italia, Luciana Lamorgese.
Viongozi wengine walioshiriki mkutano huo walikuwa ni Naibu Waziri İsmail Çataklı, Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Pwani Meja Ahmet Kendir, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Savaş Ünlü na Mkuu wa Idara ya Jumuiya ya Ulaya na Uhusiano wa Kigeni Sezer Işıktaş.
Katika mkutano huo uliofanyijka ndani bila ya waandishi wa habari, kulijadiliwa masuala kama vile hali ya uhifadhi wa wahamiaji, usafirishaji haramu wa binadamu na mapambano dhidi ya uhamiaji wa kiholela.

No comments:
Post a Comment