Na John Walter-Babati
Uongozi wa kampuni ya Mati Super Brand Ltd wilayani Babati mkoani Manyara wakiongozwa na mkurugenzi wa kampuni David Mulokozi, wamefanya tendo la huruma kwa kutoa msaada wa vitu mbalimbali katika Kituo cha Watoto Yatima cha Hossana Home care Foundation kilichopo kijiji cha Managha kata ya Singe mjini Babati.
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada kituoni hapo Desemba 24, 2020 Mkurugenzi wa Mati Super Brand David Mulokozi alisema wamefanya hivyo ikiwa ni sehemu ya kampuni hiyo inayojihusisha na uzaishaji wa pombe Kali na bidhaa nyingine kusaidia kundi hilo lenye uhitaji katika jamii ili waweze kufurahia siku kuu ya Krismas.
Miongoni mwa vitu walivyopatiwa watoto hao ni pamoja na mchele, maharage, Mahindi, mafuta ya kupikia, sukari, chumvi, dagaa, majani ya chai, juisi, Viatu, nguo, madaftari na kalamu, sabuni na vifaa vya usafi.
Kwa upande wa uongozi wa Kituo hicho, waliushukuru uongozi wa kampuni hiyo kwa kutambua uhitaji wa watoto wa Kituo hicho na kuomba makundi mengine kutosita kujitokeza kusaidia watoto hao.
Kituo hicho kilianzishwa mnamo mwaka 2019.

No comments:
Post a Comment