Rais Donald Trump amesema awamu ya kwanza ya chanjo hiyo itapewa wafanyakazi wa White House waliyo na mahitaji maalum ya kiafya
Maafisa wa ngazi ya juu katika utawala wa Trump watakuwa miongoni mwa watu wa kwanza watakaopewa chanjo ya corona, maafisa nchini Marekani wamesema.
Maafisa wamesema baadhi ya wafanyakazi wa White House wanatarajiwa kupewa chanjo ya Pfizer/BioNTech wiki hii.
Lakini siku ya Jumapili, Rais Donald Trump alisema chanjo ya mapema itatolewa kwa watu maaluma.
Chanjo hiyo inatoa ulinzi wa hadi asilimia 95 dhidi ya Covid-19 ana inaidhinishwa kuwa salama na wadhibiti wa dawa wa Marekani iliyopita Ijumaa.
Dozi milioni tatu za kwanza za chanjo hiyo kwasaba zinasambazwa katika maeneo tofauti katika majimbo yote 50 ya Marekani.
Shehena ya kwanza ya dozi hizo iliwasilishwa Michigan siku ya Jumapili, wahudumu wa afya na wazee ndia wanaotarajiwa kupewa mapema Jumatatu.
Vifo vilivyotokana na corona vimeongezeka sana mwezi Novemba nchini Marekani, ikivunja rekodi duniani kwa kuwa na idadi ya juu zaidi ya maambukizi ya 3,309 siku ya Jumamosi.
Lakini kuzinduliwa kwa mpango wa chanjo kunachukuliwa kuwa hatua kubwa katika mapambano dhidi ya janga la corona, ambalo limesababisha vifo vya watu 300,000 Marekani.

No comments:
Post a Comment