Search This Blog

Friday, December 18, 2020

Haruna Niyonzima: Tutachukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara


 BAADA ya kusaini dili la mwaka mmoja kiungo fundi wa kuchezea mpira, Haruna Niyonzima amesema kuwa anaamini timu hiyo itatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara. 

Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 37 baada ya kucheza jumla ya mechi 15.

Imeshinda mechi 11, sare nne na haijapoteza mchezo, ikiwa imefunga mabao 22, Niyonzima amefunga bao ilikuwa ni Uwanja wa Mkapa wakati Yanga ikishinda mabao 3-0.

Niyonzima ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Yanga hivyo ataendelea kupambana mbele ya Kocha Mkuu,  Cedric Kaze. 

Nyota huyo amesema:"Nipo Yanga kwa sasa na ninafuraha kubwa, imani yangu ni kuona kwamba tunatimiza malengo tuliyojiwekea ili kufikia malengo tuliyojiwekea

"Tunahitaji ubingwa na hilo lipo wazi, tunaamini kwamba tutafikia malengo hayo," .



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...