Watu 2 wamerşpotiwa kufariki na wengine 3 kujeruhiwa vibaya kwenye ajali ya helikopta iliyotokea katika mji wa Kaikoura kaskazini mashariki mwa Kisiwa cha Kusini cha New Zealand.
Kulingana na taarifa za gazeti la New Zealand Herald, helikopta hiyo iliyokuwa imebeba watu 5 wakiwemo watoto, ilianguka kwenye maporomoko karibu na eneo la Clarence kaskazini mwa mji.
Watu 2 waliokuwemo kwenye helikopta walifariki katika ajali hiyo, na wengine 3 wakajeruhiwa vibaya.
Hapo awali, shughuli ya uokoaji wa waathiriwa ilianzishwa na wenyeji wa mkoa huo, na baadaye timu ya wazima moto, vikosi vya polisi na helikopta za wagonjwa kutoka Christchurch, Nelson na Wellington zikatumwa kwenye eneo la ajali.
Shirika la Usafiri wa Anga la New Zealand liliripoti kuwa chanzo cha ajali hiyo kinafanyiwa uchunguzi.

No comments:
Post a Comment