Search This Blog

Thursday, November 19, 2020

Watu saba wafariki dunia wakidai kuachiliwa huru kwa Bobi Wine


Idadi ya waaandamanaji waliofariki dunia wakati wa maaandamano ya Jumatano ya kupinga kukamatwa kwa Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, imeongezeka na kufikia saba, polisi imesema.

Msemaji amezungumza na BBC Alhamisi asubuhi na kusema kuwa zaidi ya waandamanaji 40 walijeruhiwa katika makabiliano na polisi.

Shirika la Msalaba Mwekundu Uganda linasema kuwa wafanyakazi wake waliwasaidia watu 11 waliokuwa na majeraha ya kupigwa risasi.

Wakati huohuo, upinzani umesitisha kampeni zake kushinikiza kuachiliwa huru kwa Bobi Wine.

Waliokuwa majenerali wa jeshi Mugisha Muntu na Henry Tumukunde pia wametaka polisi kusitisha unyanyasaji dhidi ya wagombea urais wa upinzani na raia.

Polisi imesitisha matukio kadhaa ya kampeni ya wagombea wa upinzani.

Bobi Wine alikamatwa katika mkutano wake wa kampeni mashariki mwa Uganda.

Polisi walimbeba Bobi Wine na kumuweka kwenye gari lao wakidai kuwa amevutia umati mkubwa wa watu zaidi ya 200, kuliko idadi iliyopendekezwa na Tume ya Uchaguzi kama njia moja ya kukabiliana na virusi vya corona.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...