Search This Blog

Tuesday, November 17, 2020

Watatu wahukumiwa miaka 30 jela, walipora kwa kutumia silaha


Petro Mlongo (29), Masumbuko Sakumi (25) na Jackson Masumbuko (26) wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kukutwa na hatia kwenye kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha.

Walitumia panga kumjeruhi kichwani na mgongoni Zwiyo Mpemba huku wakimpora Tsh. 300,000 pamoja na simu mbili ambazo zote zina thamani Tsh. 120,000.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Geita, Sosthenes Kiiza amesema adhabu kali imetolewa kwa watatu hao kama fundisho kwa wengine wenye tabia za ukatili wa aina hiyo.

Watatu hao wameomba kupunguziwa adhabu wakisema wazazi wanawategemea lakini Hakimu Kiiza ametupilia mbali utetezi wao.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...