Search This Blog

Tuesday, November 17, 2020

Rais wa Azerbaijan atembelea miji iliyokombolewa kutoka kwa Armenia


Rais wa Azerbaijan  Ilham Aliyev ametembelea miji ya Fuzuli na Jabrail, ambayo imekombolewa kutoka kwenye uvamizi wa Armenia.

Katika picha zilizorushwa na mke wa Ilham Aliyev, Mihriban Aliyeva kwenye ukurasa wa Instagram, inaonekana kuwa Rais Aliyev alifanya ziara hizo kwa gari lake.

Aliyev amesema kwamba wako katika mkoa wa Jibrael na wanaenda katika mwelekeo wa Daraja la Hudaferin la kihistoria.

Aliyev, akionyesha nyumba zilizoharibiwa akiwa akikuzunguka, alisema,

"Hizi ni nyumba za raia wa Azerbaijan  zilizoharibiwa na adui katili."

Aliyev alipofika Mto Araz, alisema,

"Huu ni mpaka wa Azabajani na Iran; ni mpaka wa urafiki,"

Kati ya picha zilizorushwa kwenye mitandao ya kijamii, kuna moja Ilham Aliyev ameonekana akibusu na kupandisha bendera ya Azerbaijan.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...