Search This Blog

Monday, November 16, 2020

Wafuasi wa Bobi Wine watawanywa kwa vitoza machozi Uganda


Wafuasi wa mgombea urais ambaye pia ni mwanamuziki Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, wamerushiwa vitoza machozi na polisi Jumapili nchini Uganda, pamoja na kumkataza mgombea huyo kuingia kwenye eneo alilopanga kufanya kampeni.

Wafuasi wa Bobi Wine walikuwa wamekusanyika katika mji wa Kumi, mashariki mwa nchi hiyo walipotawanywa.

Msafara wake baadaye ukakatazwa kuingia katika eneo la Sironko na kulazimika kurejea mji wa Mbale ambapo wafuasi wake walifyatuliwa vitoza machozi.

Bobi Wine aliweka picha za makabiliano kati ya polisi na wafuasi wake kwenye mtandao wa Twitter:

Rais Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani kwa zaidi miongo mitatu anatafuta kuchaguliwa tena.

Pia miongozo ya wizara ya afya inapinga wanasiasa kukusanyika na makundi makubwa ya wafuasi yao, badala yake, kuhutubia umati wa watu usio zidi 70.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...