Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa limeiambia BBC kuwa maelfu ya raia wanaendelea kukimbilia nchini Sudan wakitoroka vurugu zinazoendelea kundirima kaskazini mwa Ethiopia eneo la Tigray.
Mwakilishi wa Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) nchini Sudan, Axel Bisschop, amesema wengi wao ni familia zinazotoroka ghasia na wanatembea kwa miguu kwasababu hali katika eneo la Tigray inaendelea kuwa ya hatari zaidi.
Hata hivyo Ethiopia imekanusha madai kuwa inalenga raia wasio na hatia wakati ambapo inaendelea na kampeni yake dhidi ya chama cha Tigray People's Liberation Front (TPLF).
Vikosi vya serikali vimesema vinaendelea kuingia katika mji wa Mekelle, ingawa imekuwa vigumu kuthibitisha taarifa hizo kwasababu ya kukatizwa kwa mawasiliano.
Hadi kufikia sasa, zaidi ya raia 30,000 wamevuka mpaka na kuingia nchini Sudan.

No comments:
Post a Comment