Watu 20 wameripotiwa kupoteza maisha kwenye ajali iliyotokea magharibi mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari vya kitaifa, iliarifiwa kuwa lori moja liliingia sokoni kwenye eneo la Akungba Akoko lililoko mkoani Ondo na kukanyaga umati.
Watu 20 walipoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa katika ajali hiyo.
Majeruhi walifikishwa katika hospitali za karibu kwa ajili ya matibabu.
Bado kuna hali ya wasiwasi kuhusiana na idadi ya vifo inayohofiwa kuongezeka.

No comments:
Post a Comment