Search This Blog

Sunday, November 15, 2020

Hamilton aifikia rekodi ya Schumacher ubingwa wa 7


Lewis Hamilton ameshinda ubingwa wa dunia wa mbio za magari 'Formula1' mwaka 2020, baada ya kuongoza mbio za Uturuki (Turkish Grand Prix), zilizomalizika mchana wa leo Novemba 15, 2020.


Hamilton ambaye ni derewa wa timu ya magari ya Mercedes, sasa amechukua ubingwa huo kwa mara ya 7 na kuifikia rekodi ya nguli Michael Schumacher.


LEWIS: "It's so important for kids out there to see this...


"Don't listen to anyone who tells you you can't achieve something. Dream the impossible. Speak it into existence. You've got to work for it, chase it, and never give up!"#TurkishGP  #F1 pic.twitter.com/aZMVSw1j5j


— Formula 1 (@F1) November 15, 2020


Raia huyo wa Uingereza mwenye miaka 34, ameshinda ubingwa zikiwa zimebaki mbio mbili kukamilisha msimu wa 2020. Mbio zilizobaki ni za Bahrain (Sakhir Grand Prix) ambazo zitafanyika Desemba 4 huku zile za mwisho zikiwa ni Yas Marina, Abu Dhabi (Abu Dhabi Grand Prix) ambazo zitafanyika Ijumaa Desemba 11.

Katika mbio za leo za Uturuki, Lewis ameongoza huku dereva mwenzake kutoka timu ya Mercedes Valtteri Bottas.


Lewis Hamilton - Mercedes

Sergio Perez - Racing Point

Sebastian Vettel - Ferrari

Charles Leclerc - Ferrari

Carlos Sainz - McLaren

Max Verstappen - Red Bull

Thailand Alexander - Red Bull    

Lando Norris - McLaren

Lance Stroll - Racing Point

Daniel Ricciardo - Renault


Lewis Hamilton amechukua ubingwa huo mwaka 2008, 2014, 2015, 2017, 2018, 2019 na 2020.

Schumacher yeye amechukua ubingwa mwaka 1994, 1995, 2000, 2001, 2002, 2003 na 2004



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...