Rais wa Zanzibar Mh.Hussein Mwinyi amesema mpaka sasa chama cha ACT Wazalendo hawajapeleka jina la Makamu wa kwanza wa Rais kama katiba inavyotaka baada ya kupata zaidi ya asilimia 10 ya kura zilizopigwa na ndioa maana nafasi hiyo iko wazi mpaka sasa
"Baada ya kukamilika kwa uchaguzi na ACTwazalendo kupata zaidi ya 10% tuliwaandikia barua ili walete jina la Makamu wa kwanza wa Rais jina bado halijafika na nimeacha nafasi 2 za mawaziri wa chama cha ACT Wazalendo endapo watakuwa tayari."- Dkt. Mwinyi

No comments:
Post a Comment