Kama kichwa cha Habari kinavyojielezea mimi ni binti mrembo tu Nina kaxi yangu nzuri Namshukuru Mungu, nimepita kwenye mahusiano kadhaa changamoto hazikosekani Nimekutana na wenye uwezo wanaoweza kanipa Nitakacho na wenye uwezo wa kawaida tu.
Nilichojifunza ni kwamba Unaweza kuwa kwenye mahusiano na mtu Anaejiweza akakupa kila utakacho ila hana muda na wewe hamna out wala muda wa kukaa mkayajenga hata mazungumzo ya kawaida maana mimi ni mpambanaji
Mkikutana ni show basi siku zinaenda mwaka umekatika hamna la maana na sio kwamba anamahusiano mengine Hapana ingawa Mwanaume huwezi msemea ila ni mtu ambaye uko nae huru ila yuko busy muda wote hawezi kujenga muda kwa ajili yako ila muda wa kufanya mengine kama kwenda Bar, karaoke nk anao
Pili Mwanaume Ambae hawezi kukuhudumia kwa chochote mnapata muda wa kuzungumza kushauriana kupanga Mambo ya maendeleo ingawa hamuwezi kwenda out nk kutokana na kipato ila mapenzi mnayafurahia hata kwa kukaa ndani tu coz mimi sio mtokaji na haijawahi kunipa chochote wala sijawahi kumuomba coz namjua Hali yake
Ingawa ana wasiwasi na mimi kutokana na uwezo wake na urembo wangu ila mimi sina tatizo coz najimudu kwa kila kitu. sasa huyo mwenye uwezo miezi4 hatuko vizuri na naona nimeshindwa mimi kwa moyo mweupe coz sijawahi kuenjoy nae hata siku moja nataka kumpokea huyu wa Hali ya kawaida kwa moyo mmoja tujenge familia maana kule naona utumwa naombeni Ushauri ndugu zangu
By Vantz
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment