Search This Blog

Sunday, September 13, 2020

Waziri Mkuu wa Ugiriki: Nipo tayari kufanya mazungumzo na rais wa Uturuki

 


Waziri Mkuu wa Ugiriki Kyriakos Mitsotakis amesema kuwa yupo tayari kufanya mazungumzo na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan.

Kyriakos Mitsotakis , katika mkutano na waandishi wa habari huko Thesaloniki, amezungumzia juu ya uhusiano na Uturuki na mvutano mashariki mwa Mediterania.

Mitsotakis  amesisitiza kuwa kurejea kwa Oruc Reis Antalya ni"hatua nzuri ya kwanza" na kwamba mwendelezo wa hilo ni kwamba yupo tayari kwa mazungumzo mapya na Uturuki.

"Tumeona hatua nzuri hapo awali, hatua hasi zimechukuliwa." aliongeza kiongozi huyo.

Mitsotakis  pia amedai kwamba "silaha katika visiwa vya Aegean si mada ya kuzungumziwa na haitajadiliwa".

Mitsotakis , juu ya maswali juu ya Rais Erdoğan, amesema,

"Niko tayari kukutana na Erdogan ikiwa mvutano utatuliwa."

Mazungumzo ya mwisho kama hayo kati ya nchi hizo mbili, yaliyoanzishwa mnamo 2002, yalifanyika Athene mnamo 1 Machi 2016. Baada ya tarehe hii, mazungumzo kati ya nchi hizo mbili yaliendelea kwa njia ya mashauriano ya kisiasa, lakini hayakurejea kwenye mfumo wa uchunguzi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...