Search This Blog
Monday, September 7, 2020
Saed Kubenea apandishwa kizimbani, Akosa dhamana na Kurudishwa rumande
Mbunge wa Jimbo la Ubungo aliyemaliza muda wake Saed Kubenea amepandishwa kizimbani mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Arusha akituhumiwa kwa makosa mawili likiwemo la kutatisha fedha na kuziingiza nchini bila kibali.
Akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Martha Mahumbuga jopo la mawakili wanne wa serikali wameeleza kuwa mnamo tarehe tano mwezi wa tisa huko Namanga mpakani mwa Tanzania na Kenya mtuhumiwa alikutwa na dola za Kimarekani 8000 hela za Kenya 491,700 na fedha za Kitanzania 71,000.
Mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kukiuka sheria za kuvuka mpaka kwenda nchi jirani ya Kenya na kurejea nchini Tanzania kwa kutumia njia zisizo rasmi.
Kutokana na kosa la kutakatisha fedha kutokuwa na dhamana mtuhumiwa amepelekwa gerezani hadi tarehe 21/09/2020 kesi hiyo itakapotajwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment