Search This Blog
Monday, September 7, 2020
KMC Yaanza Ligi Kuu Kwa Kichapo Cha 4-0 Dhidi ya Mbeya City
TIMU ya KMC FC leo Septemba 7 imeweza kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 mbele ya Mbeya City kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Uhuru.
Mchezo wa leo umekusanya mabao mengi kuliko mechi zote zilizochezwa jana Septemba 6 ambapo pazia la ligi lilifunguliwa rasmi .
Mabao ya KMC yalipachikwa dakika ya 21 kupitia kwa Israel dakika ya 21 akimalizia pasi ya Emmanuel Mvuyekule.
Bao la pili lilipachikwa dakika ya 39 na Hassan Kabunda kwa pasi ya Israel na kuwafanya KMC kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili KMC waliendeleza moto wao ambapo dakika ya 57, Abdul Hilary alipachika bao la tatu kwa pasi ya David Bryson na msumari wa mwisho ulipachikwa na Paul Peter dakika ya 74 kwa pasi ya Kabunda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment