Rais wa Uturuki Recep Tayyıp Erdoğan azungumza kwa njia ya simu na katibu mshauri wa Umoja wa Ulaya Charles Michel.
Tarrifa zilizotolewa na kitemgo kinachohusika na mawaislinao ikulu ya rais mjini Ankara zimefahamisha kuwa viongozi hao wamejadili inayoendelea katika ukanda wa Mediterania Mshariki.
Katika mazungumzo yao rais Erdoğan na Charles Michel wamezungumza pia kuhusu ushirkiano kati ya Uturuki na Umoja wa Ulaya.
Rais Erdoğan ameendelea akisema kwamba matamshi ya baadhi ya wanasiasa wa Ulaya kuhusu hali iliopo katika ukanda wa Mediterania Mashariki ni ishara tosha kwa Umoja wa Ulaya kutambua na kufahamu kiwango cha haki na mshikamano katika ukanda mzima.
Rais wa Uturuki amemalizia akitoa wito kwa mataifa wanachama wa Umoa wa Ulaya kuwa katika usawa kunako mzozo wa Mediterania na kutafuta suluhisho lililo la haki kwa pande zote zinazovutana.

No comments:
Post a Comment