Search This Blog
Sunday, September 13, 2020
Lebanon imeizuia ndege ya Uturuki kutua Beirut
Mamlaka nchini Lebanon imeizuia ndege ya mizigo ya Uturuki ambayo ilipaswa kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Rafik Hariri, baada ya ndege hiyo kupita katika eneo la anga la Israel.
Akinukuu vifungu vya sheria za Lebanon, Mkurugenzi wa uwanja wa ndege Fadi Al-Hassan amesema mamlaka ya uwanja wa ndege imeizua ndege hiyo kutua kwa vile ilifanya kosa la kupitia anga ya Israel, eneo la waloezi nchini Israel.
Hata hivyo aliongeza kusema hakuna matatizo zaidi na upande wa Uturuki na serikali ya Lebaon, imeelewa kwamba kitendo hicho kimetokea kwa makosa. Lebanon na Israel kwa hivi sasa zipo katika makabiliano ya kivita, na katika eneo la mpakani kumekuwa na hali ya kuongezeka kwa mvutano kati ya kundi la Hezbollah na jeshi la Israel.
Hezbollah lina uhusiano na hasimu mkubwa wa Israel, Iran. Na mwaka 2006 kulitokea vita vilivyodumu kwa mwezi mmoja kati ya kundi hilo la Isreal.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment