Search This Blog

Sunday, August 30, 2020

Waisrael waendelea kumpinga Netanyahu

Maelfu ya Waisrael wamefanya maandamano hapo jana mjini Jerusalem, ikiwa ni muendelezo wa mikusanyiko ya kila mwishoni mwa juma katika kipindi hiki cha kiangazi, yenye lengo la kushinikiza kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, ambae anakabiliwa na kesi ya rushwa na kushindwa kulishughulikia vyema janga la virusi vya corona.

Maandamano mengine madogo, madogo yalifanyika pia katika maeneo mengine ya Israel, likiwemo la mji wa Caesaria, ambako kuna makazi binafsi ya Netanyahu.

Katika mkusanyiko mkubwa mjini Jerusalem, waandamanaji walikusanyika katika eneo la kuingilia mji huo na katika makazi rasmi ya Netanyahu, wakiwa wameshika bendera ya Israel na nyingine nyeusi ikiwa ni ishara ya moja ya harakati za kupinga.

Serikali ya muungano ya Israel hivi karibuni ilinusurika kuvunjika baada ya kushindwa kufikia makubaliano kuhusu bajeti.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...