Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuwahimiza wananchi wote wakiwemo, wakulima, wafugaji na wavuvi kutumia fursa za uwepo wa umeme wa kutosha na wa uhakika ili kujiletea maendeleo.
Hayo yamesemwa Agosti 2, 2020 na Meneja wa TANESCO mkoa wa Simiyu, Eng. Khadija Abdallahmed kwenye banda la TANESCO katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
“Naomba kutoa wito kwa watanzania wote kwa ujumla wachangamkie hizi fursa za umeme na maendeleo ya kilimo, mifugo na uvuvi Tanzania nzima, umeme upo wa kutosha Tanzania nzima, TANESCO tupo tunaaangaza maisha.” Alisisitiza Eng. Khadija
Alisema TANESCO inashiriki maonyesho haya kwa vile wao ni wadau wakubwa wa shughuli za kilimo, mifugo pamoja na uvuvi na kwa huduma ya umeme itolewayo na shirika hilo ni sehemu ya kufanikisha maonesho hayo.
Aliwakaribisha wananchi wote wanaopata fursa ya kufika kwenye viwanja vya Nyakabindi yanakofanyika maonesho hayo kutembeela katika banda la TANESCO kwani watafaidika na kupata elimu kuhusu matumizi bora na sahihi ya umeme.
“Lakini wananchi watakaofika kwenye banda letu watakutana na mtaalamu mbobezi ambaye atawaeleza kuhusu mradi mkubwaj wa kimkakati wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme Julius Nyerere (JNHPP 2115) kwenye bonde la mto Rufiji.” Alisema.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...
No comments:
Post a Comment