Search This Blog

Wednesday, August 19, 2020

Kizza Besigye ajiondoa rasmi kwenye kinyang'anyiro cha urais Uganda

 Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Dr. Kizza Besigye amewaambia wafuasi wake kwamba hatagombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2021.


Alikuwa akizungumza katika ofisi za chama cha Forum for Democratic Change katika siku za mwisho za uteuzi wa wale wanaogombea urais katika chama hicho .


Besigye ambaye aliwahi kuwa daktari wa maungo wa rais Museveni alimpinga Museveni mara nne katika uchaguzi tangu 2001 lakini akapoteza mara zote hizo.


Hatahivyo amedai kwamba uchaguzi huo ulikumbwa na udanganyifu. Alienda mahakamani kupinga matokeo hayo mwaka 2006 na 2011 katika mahakama ya juu lakini jaji akaidhinisha matokeo hayo.


Basigye awali alikataa kuzumgumza hadharani iwapo atawania uchaguzi lakini katika siku za hivi karibuni alisema kwamba taifa linafaa kumuunga mkono kiongozi wa mpito ambaye atamuunga mkono.


Uamuzi wa Dkt. Besigye wa kutogombea urais mwaka 2021 umekiacha chama cha FDC kikimtafuta atakayekiwakilisha katika uchaguzi huo.


Tayari chama hicho kimeahirisha mara mbili uteuzi wa wagombea wake wa urais kwa matumaini kuwa Dkt. Besigye angebadili msimamo wake na kuchukua fomu za uteuzi.



2019 mbunge wa upinzani Uganda Robert Kyagulanyi na mwanaharakati wa kisiasa pamoja na Dkt Kizza Besigye waliahidi kushirikiana kukiondosha madarakani chama tawala National Resistance Movement (NRM) kinachoongozwa na rais Yoweri Museveni.


Chama tawala cha NRM kimekuwa madarakani tangu 1986.


Akizungumza na kituo cha televisheni cha NTV, Bwana Besigye alikataa kujibu swali juu ya iwapo atagombea urais 2021 au la.


Mara nyingi alisisitiza kuwa swali hilo ni kosa. Alisema hakuna uchaguzi utakaomng'oa madarakani Rais Museveni.


"Hatuhitaji uchaguzi ili tupate uhuru. Mkakati unaopaswa kutuandaa kupigana kwa ajili ya nchi yetu uchaguzi uwepo au la," alisema Dkt Besigye ni mpiganaji wa zamani na daktari binafsi wa Museveni wakati wa vita vyao vya msituni vya kati ya mwaka 1981 hadi 1986 vilivyoweka madarakani vuguvugu la National Resistance Movement (NRM).



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...