Search This Blog
Tuesday, August 4, 2020
Huyu Hapa Mgombea Aliyepitishwa Kugombea Urais Zanzibar, Salum Mwalim Awa Mgombea Mwenza
Baraza Kuu la CHADEMA limempitisha Said Issa Mohamed kuwa mgombea Urais wa chama hicho Zanzibar.
Said ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Zanzibar) amepitishwa kwa kura za ndiyo na wajumbe zaidi ya 500 huku wajumbe watano wakimpigia kura za hapana.
Baraza Kuu la CHADEMA limempitisha Salum Mwalim Juma kuwa Mgombea mwenza wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Salum Mwalim ambaye pia Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar amepitishwa kwa kura za ndiyo na wajumbe zaidi ya 500 huku wajumbe wannne wakimpigia kura za hapana.
Salum Mwalim sasa atasubiri jina la mgombea urais atakayepitishwa na chama hicho ili aweze kuwa mgombea wake mwenza.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment