Search This Blog

Saturday, August 15, 2020

Hasunga Atoa Siku 5 Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Kukamilisha Malipo ya Wakulima wa Korosho Kibiti na Mkuranga

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga ametoa siku

Tano kwa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania(CPB), Viongozi wa Vyama

vya Ushirika pamoja na Benki ya Kilimo, kuhakikisha wanakutana na wakulima wa

Korosho Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani ambao fedha zao za mauzo ya Korosho

hazijalipwa mpaka sasa ili kuwalipa haraka iwezekanavyo.


Amewataka kukagua taarifa zao na kuwalipa

fedha zao mara moja kwani serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania Dkt

John Pombe Magufuli ilishatoa fedha zote kwa ajili ya kufanyika kwa malipo hayo, “Nasikitika kwanini mpaka sasa malipo hayajakamilika” Aliuliza Waziri Hasunga


Akizungumza mbele ya Wakulima na Maafisa ugani Waziri Hasunga amesema kuwa inasikitisha kuona bado kuna wakulima wanaidai serikali

angali serikali kupitia kwa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli imekwisha kutoa

fedha kwa ajili ya kuwalipa kwa muda mrefu kitendo kinachowafanya wakulima

kuichukia serikali na kukata taama ya kufanya kilimo.


Amesema kuwa kumekuwa na kisingizio cha muda mrefu kuwa baadhi ya wakulima taarifa

zao za kibenki zina makosa hivyo kusababisha kushindwa kufanyiwa malipo kwa

njia ya kibenki jambo hili siwezi kukubaliana nalo.


“Nilitoa siku 14 kuhakikisha kuwa wakulima wa

Korosho Wilaya ya Mkuranga wawe wamemaliza kulipwa fedha zao lakini mpaka sasa

bado natoa siku tano Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko

Tanzania(CPB), viongozi wa Vyama vya Ushirika pamoja na Benki ya Kilimo

kuhakikisha hili suala linamalizika” Alisema Hasunga


Aidha, Hasunga ametoa siku mbili

kwa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania CPB kuhakikisha

wanabandika majina ya Wakulima waliolipwa fedha zao za Korosho kuanzia Mwezi

Januari 2020 kwenye mbao za matangazo ili kuwasaidia wakulima kutambua

walikwisha kulipwa fedha zao na ambao bado ili pia serikali kuweza kubaini

udanganyifu unaofanywa katika malipo.


Pia amesema serikali kupitia Wizara ya Kilimo

na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga imewakamata na itaendelea kuwakamata

viongozi wa vyama vya ushirika wanaofanya ubadhilifu wa mali za wanaushirika,

pia na waliofanya ubadhilifu na wizi kwenye uuzaji wa Korosho msimu uliopita


Hivyo, Hasunga amewataka wakulima kuendelea

kuvumilia wakati  serikali ikiendelea kuwafuatilia na kuwakamata

waliofanya wizi wa kuuza korosho za wakulima bila kufuata utaratibi na kuwalipa

Wakulima hao.


Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga mbali na

kutembelea, kusikiliza na kutatua kero za Wakulima wa Korosho Wilayani Mkuranga

Mkoani Pwani alifika pia kuzungumza na wakulima Wilayani Kibiti Mkoani hapo

huku akiendelea kutoa maagizo ya kuhakikisha wakulima wa Korosho wanalipwa

stahiki zao kwa wakati na waliofanya udanganyifu na kuuza korosho za wakulima

kuchukuliwa hatua za Kisheria.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...