Search This Blog
Friday, August 28, 2020
CHADEMA wazindua kampeni, Lissu azungumza haya
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Leo Agosti 28, 2020, kimefanya uzinduzi wa kampeni za mgombea Urais kwenye viwanja vya Mbagala Zakhiem, ambapo Mgombea wa Kiti hicho cha Urais Tundu Lissu amesema, wanaanza kampeni wakiwa hawana wagombea 52 kati ya wagombea 244 waliowaweka.
Katika uzinduzi huo Lissu amesema kuwa hawategemei kujitoa kwenye uchaguzi na kwamba kuanzia leo katika kila mkutano wa kampeni hoja yao kubwa itakuwa ni ya kurudishwa kwa wagombea waliondolewa bila kuwekewa masharti yoyote.
"Hatutajitoa kwenye uchaguzi, tutakachofanya kuanzia leo nchi nzima, katika kila mkutano wa kampeni hoja yetu ni wagombea wetu walioondolewa kinyume cha sheria warudishwe bila masharti yoyote na hata wa vyama vingine warudishwe", amesema Lissu.
Aidha amesema kuwa hoja zao siyo kwa wagombea wa CHADEMA tu, bali hata vyama vingine ambavyo wagombea wao wameenguliwa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment