Search This Blog
Tuesday, August 18, 2020
20 Percent : Narudi Kwenye Muziki Kuondoa Mziki wa Matusi Uliotawala
Baada ya kimya cha muda mrefu Mwanamuziki 20 Percent aliibukia na kutumbuiza katika tamasha la Chama cha Mapinduzi lililofanyika katika Uwanja wa Uhuru siku ya Jumamosi
Baada ya kumaliza kutumbuiza amesema anafarijika kuona bado mashabiki wake wana upendo naye na bado anaishi mioyoni mwao kwani alipotumbuiza mashabiki wengi walimshangilia sana
Akihojiwa kutokana na mabadiliko ya muziki wa sasa akirejea atabadilika au ataendelea kufanya muziki wake wa zamani, 20 Percent ameahidi kurejea na kuleta muziki wa heshima na kukimbiza muziki wa matusi aliodai umetawala kwa sasa
Aidha, akihojiwa kuhusu kufanya muziki kuendana na soko la sasa, 20 Percent amesema “Mimi silengi soko, nalenga fikra za mlalahoi na mtu yeyote ambaye huzuni yake ipo na hamna mtu wa kuiongelea.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment