Search This Blog
Monday, July 13, 2020
WHO yasema mataifa yanachukua mkondo mbaya
Maafisa wa WHO wanasema kwamba haiwezekani kwamba chanjo ya corona itapatikana hivi karibuni
Janga la corona litakuwa ''baya na baya zaidi'' ikiwa serikali zitashindwa kuchukua hatua madhubuti, Shirika la afya duniani (WHO) limetahadharisha.
Mkuu wa shirika hilo Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema ''nchi nyingi sana (zilikua) zikielekea kwenye njia isiyo sahihi.''
''Idadi ya watu walioambukizwa ilikuwa ikiongezeka kwenye maeneo ambayo masharti yalikuwa hayafuatwi'', aliongeza.
Marekani imeshuhudia ongezeko la maambukizi wakati kukiwa na mvutano kati ya wataalamu wa afya na Rais Donald Trump.
Marekani, nchi iliyoathirika zaidi duniani, ina watu zaidi ya milioni 3.3 walioathirika na vifo zaidi ya 135,000 kwa mujibu wa Chuo cha Johns Hopkins.
Katika mkutano wa siku ya Jumatatu , Dkt Tedros amesema ''ujumbe mchanganyiko kutoka kwa viongozi'' umekuwa ukishusha uaminifu wa Umma katika jitihada za kudhibiti janga la virusi vya corona.
''Virusi vinaendelea kuwa adui wa kwanza wa watu, lakini hatua za serikali nyingi na watu hazioneshi hilo,'' alisema.
Dkt Tedros amesema kuwa hatua kama vile ya kukaa mbali na mwingine, kunawa mikono na kuvaa barakoa katika mazingira yanayolazimu kufanya hivyo zilipaswa kuzingatiwa kwa kiasi kikubwa, akitahadharisha kuwa kutakuwa na ''hakuna kurejea kwenye maisha ya zamani siku za usoni''.
''Ikiwa vitu vya msingi havifuatwi, kuna njia moja janga hili litaelekea,'' dkt aliongeza: ''hali itakuwa mbaya na mbaya sana.''
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment