Search This Blog

Tuesday, July 28, 2020

Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia, Najib Razak kukata rufaa dhidi ya kifungo cha miaka 12


Waziri Mkuu wa zamani wa Malaysia Najib Razak amesema kuwa atakata rufaa dhidi ya hukumu iliyomkuta na hatia ya ufisadi, na kumpa adhabu ya kifungo cha miaka 12 jela.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya hukumu ya korti ya juu hii leo, Razak amesema hakuridhishwa na namna mahakama hiyo ilivyohitimisha kesi dhidi yake, na kuongeza kuwa atakata rufaa bila kukawia.

Razak amekutwa na hatia katika mashtaka yote saba ya ufisadi yaliyokuwa yakimkabili, kuhusiana na kashfa ya mabilioni ya dola yaliyokuwa yametolewa na serikali kwa ajili ya mradi wa maendeleo.

Hukumu hiyo ilichukuliwa kama kipimo kwa utawala wa sheria nchini Malaysia, kwani imetolewa miezi mitano tu baada ya muungano unaokijumuisha chama cha Razak kushinda uchaguzi, ambapo wengi walihofu kuwa ushindi huo ungeshawishi uamuzi wa mahakama.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...