Search This Blog
Friday, July 24, 2020
Mwanamke Akiri Kumdunga Kisu Mumewe Kufuatia Mabishano ya Meseji iliyoingia Kwenye Simu
Anaidaiwa kukimbia jikoni na kuchukua kisu kabla kumdunga mumewe kifuani na kumsukuma ukutani. Hisani.
Mwanamke aliyekamatwa na kufikishwa kortini baada ya kumdunga mumewe kisu tumboni wakikangangania simu amekiri makosa na kujitetea.
Mary Nduta alikiri kumdunga kisu mumewe Solomon Njoroge Maingi nyumbani kwao katika mtaa wa Mwiki, Kasarani Nairobi Julai 19.
Akizungumza mbele ya hakimu mkazi David Ndungu katika mahakama ya Mlimani, Nduta alieleza kuwa alimdunga kisu mumewe kama njia ya kujikinga baada ya kuzidiwa nguvu.
Mlalamishi, Solomon Njorogo Maingi anaendelea kupata matibabu katika hospitali kuu ya Kenyatta alikolazwa baada ya mkasa huo.
Njoroge alirudi nyumbani baada ya wiki mbili na mkewe kuanza kulalamika kuhusu jinsi mumewe wa kwanza alivyokuwa akimpa pesa nyingi kumshinda..
Njoroge alijua kuwa alikuwa katika mawasiliano na mume huyo na hivyo akataka kuona simu, hapo ndipo majibizano yalianza .
Nduta anaidaiwa kukimbia jikoni upesi na kuchukua kisu kabla kumdunga mumewe kifuani na kumsukuma ukutani.
Njoroge aliokolewa na jirani ambaye alifika upesi na kumtolea kisu hicho kifuani kabla kumkimbiza hospitalini kwa matibabu.
Mwanamke huyu alinaswa na maafisa wa polisi waliopata kisu pamoja na nguo ya kulala katika chumba chao cha kulala zikiwa na matome ya damu.
Nduta aliachiliwa kwa dhamana ya KSh 100,000 huku kesi yake ikisubiriwa kutajwa tena Agosti 4, 20202.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment