Search This Blog
Thursday, July 2, 2020
Mgonjwa wa 91' aliyezua hofu katika taifa zima la Vietnam
''Iwapo angekuwa katika eneo lolote jingine , angekuwa amefariki. Wangezima mashine ya kumsaidia kuishi baada ya siku 30'', anasema Stephen Cameron akiwa katika kitanda chake cha hospitali.
Raia huyo wa Uskochi mwenye umri wa miaka 43 aliishi siku 68 akiwa anasaidiwa na mashine ya kupumua .
Huu ndio muda mrefu zaidi ambao haujawahi kutumiwa na mgonjwa mwingine yeyote nchini Uingereza katika hali hiyo.
Lakini hakuwa amelazwa katika wodi ya hospitali ya Motherwell , nyumbani kwao bali katika chumba cha wagonjwa mahututi cha Ho Chi Minh, nchini Vietnam bila marafiki ama watu wake wa familia yake.
Cameron ambaye alikuwa ndie mgonjwa wa mwisho katika chumba cha wagonjwa mahututi nchini Vietnam ni mgonjwa ambaye ameugua sana nchini humo wakati wa mlipuko wa virusi vya corona.
Taifa la Vietnam lenye wageni milioni 95, lilikuwa na wagonjwa wachache waliothibitishwa kuwa na corona , huku chini ya 10 wakilazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi na hakuna kifo chochote kilichotangazwa.
Ugonjwa wa Cameron haukuwa wa kawaida nchini Vietnam hatua ambayo ilisababisha hali yake kuripotiwa kila dakika katika magazeti ya kitaifa pamoja na televisheni.
Makumi ya wataalam wa vyumba vya wagonjwa mahututi nchini Vietnam walifanya mikutano ya video ya mara kwa mara ili kujadiliana kuhusu hali ya Cameron.
"Kutokana na idadi ndogo ya wagonjwa katika vyumba vya wagonjwa mahututi, ilimaanisha kwamba kila mgonjwa aliye katika hali mahututi aliwavutia madaktari wa hali ya juu nchini '', anaelezea Dkt. Kidong Park, mwakilishi wa Shirika la afya duniani WHO nchini Vietnam.
Kwa muda wa miezi miwili na nusu Bwana Cameron alikuwa amelazwa akiwa hana fahamu, na alitegemea mashine ya oksijeni inayotumika kusaidia mtu aliye katika hali mahututi kuwa hai.
Mashine hiyo ilikuwa ikichukua damu kutoka kwa mwili wake kuichanganya na oksijeni kabla ya kuirudisha mwilini mwake.
"Nina bahati kwa kuwa tatizo langu sasa ni kushindwa kusukuma miguu yangu , lakini ninafanyiwa tiba ya viungo katika miguu yangu mara mbili kwa siku'', alisema Cameron.
"Wakati mmoja, wizara ya masuala ya kigeni ilimwambia rafiki yangu Craig kwamba nilikuwa na asilimia 10 kupona , hivyobasi akajianda kwa lolote lile.
Aliifahamisha idara niliokuwa nikifanyia kazi na kuanza kufanya kile ambacho mtu angefanya iwapo mtu angerudi nyumbani akiwa ndani ya jeneza.
Tangu alipopata fahamu , alianza mawasiliano ya simu na marafiki nyumbani kwake huko nchini Uskochi ambao hawakufikiria kwamba angerudi akiwa hai ."
Madaktari walilazimika kukabiliana na magonjwa kadhaa tofauti wakati Cameron alipokuwa amepoteza fahamu: Alikuwa na mgando wa damu, figo zake zilikuwa zimeathirika - ikimaanisha kwamba zilihitaji kusafishwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment