MJINI kuna mambooo! Juzi (Jumatano), Sinza jijini Dar es Salaam, kulikuwa na sherehe ya ‘bethdei’ ya msanii wa filamu nchini Kajala Masanja, lakini katikati ya shughuli likazuka jambo, tega sahani upakuliwe ubuyu.
Jambo lenyewe linamhusu prodyuza mahili Bongo, Paul Matthysse ‘P- Funk’ ambaye ni mzazi mwenzake na Kajala, kujikuta akipata ‘wenge’ baada ya kile kinachotajwa kuwa ni mkewe wa sasa (jina kapuni) kumaindi uwepo wake kwenye shughuli hiyo.
Baada ya kutimba kibabe kwenye sherehe hiyo, prodyuza huyo alikwenda moja kwa moja kwa EX wake na kumkumbatia ambapo ‘mama’ naye alionesha mahaba kwa kukata keki na kumlisha mzazi mwenzake.
Kitendo hicho cha P-Funk, kiliibua shangwe kwa wageni waalikwa waliokuwa wameshiriki shughuli hiyo iliyofanyika ndani ya ofisi ya Kajala iliyopo Sinza Afrikasana.
Hata hivyo, wakati shughuli ikiendelea, ghafla prodyuza huyo alipigiwa simu na mtu anayedaiwa kuwa ni mke wake akimhitaji arudi nyumbani.Chanzo cha karibu na P- Funk kiliwanong’oneza waandishi wetu kuwa, kuna wambeya kutoka shughulini hapo walikuwa wamerusha klipu ya video mtandaoni ikimuonesha Kajala na mzazi mwenzake huyo wakiwa wamekumbatiana jambo ambalo linadaiwa kumkera mke wa P- Funk.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment