Search This Blog
Wednesday, July 29, 2020
Katavi: Watu 15 wakamatwa kwa kumuozesha binti wa darasa la 5
Jeshi la Polisi limewakamata Watuhumiwa 15 wakiwemo Wazazi 2 kwa kumuozesha Mwananfunzi wa darasa la 5 kwa mahari ya ng'ombe 12
Kamanda wa Polisi wa Mkoani humo, Benjamin Kuzaga amesema wamefanikisha kuisambaratisha ndoa hiyo ya kimila na wanaendelea na juhudi za kumtafuta muoaji ambaye alitoroka
Ndoa za Utotoni, chini ya miaka 18 (Wavulana na Wasichana) ni marufuku Tanzania kutokana na kushinda kwa kesi iliyofunguliwa mwaka 2016 na Mkurugenzi wa Asasi ya Kiraia ya Msichana Initiative, Rebecca Gyumi. Awali umri wa kufunga ndoa ulitofautiana kwa Wavulana na Wasichana
Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, Kifungu cha 148 (1&2) kinasema Mtu yeyote anayefunga ndoa huku akijua au akiwa na sababu ya kujua kuwa mwenza wake yupo chini ya umri wa ndoa atahukumiwa kifungo cha miaka 3
Pia, mtu yeyote anayakeshiriki katika ndoa hiyo atakuwa na kosa na atahukumiwa kifungo kisichozidi miaka miwili
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment