Search This Blog
Monday, July 20, 2020
Kasalali aibuka mshindi kura za maoni jimbo la Sumve
Na Paschal D.Lucas,Mwanza
Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Lyoma Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza Ndugu Kasalali E.Mageni (CCM) ameibuka kidedea kwenye kinyang'anyiro cha kura za maoni kwa kupata Jumla ya kura 138 akifuatiwa na Ndugu Bujaga Moses Charles aliyekuwa na kura 131 huku namba tatu ikishikiliwa na ndugu BusigaSolwe M.Shinje aliyekuwa na kura 110.
Uchaguzi huo wa kura za maoni ulikuwa na Jumla ya Wagombea 78 na ulifanyika katika ukumbi wa Kanisa katoliki Parokia ya Nyambiti.
Wilaya ya kwimba ambayo ina Majimbo mawili ambayo ni Sumve na Kwimba ambapo katika Jimbo la Kwimba uchaguzi wa kura za maoni unatarajiwa kufanyika leo Julia, 21,2020.
Ikumbukwe Jimbo la Sumve lina miaka 25 tangu lianzishe na limeshikiliwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kipindi chote na Mbunge wake alikuwa Marehemu Richard Mganga Ndassa aliyefariki April 29,2020 Jijini Dodoma.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment