Search This Blog

Wednesday, June 17, 2020

Wafanyabiashara wa mafuta wanaoficha nishati hiyo kukiona

Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Innocent Bashungwa amesema kuwa serikali itawachukulia hatua wafanyabiashara wote wa mafuta walioficha nishati hiyo na kuacha kuuza kulingana na bei elekezi.

Waziri Bashungwa ametoa onyo hilo wakati wa kikao cha pamoja na mamlaka zinazosimamia kodi (TRA) , Nishati (EWURA) na Tume ya Ushindani (FCC) kujadili sababu na hatua zitakazochukuliwa kwa wafanyabiashara watakaobainika kwenda kinyume na sheria.

Amesema kutokana na janga la Covid-19 bei ya mafuta katika soko la dunia imeshuka huku ikichangiwa zaidi na mkakati uliowekwa wa ununuaji wa mafuta kwa pamoja, ambapo pia ametaja sheria zitakazotumika kuwakamata wanaoficha mafuta.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...