Rais wa Marekani Donld Trump anasema kwamba hatofikiria kubadilisha majina ya kambi za kijeshi zilizotajwa baada ya majenerali walioongoza jeshi la Marekani.
Alituma ujumbe wa twitter akisema kwamba kambi hizo ni miongoni mwa turathi kuu za Marekani.
Matamshi hayo ya bwana Trump yanajiri kufuatia ripoti kwamba maafisa wakuu wa jeshi walikuwa tayari kuruhusu mabadiliko kufuatia maandamano yaliosababishwa na kifo cha George Floyd.
Kwa wengi, alama za mataifa ya kusini yaliokuwa yakiwahifadhi watumwa ambayo baadaye yalijiondoa katika biashara hiyo na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe Amerika - zilikuwa na kumbukumbu za kibaguzi.
Bwana Trump alituma ujumbe wa twitter siku ya Jumatano kwamba kambi za kijeshi zilizopatiwa majina ya majenerali waliohusika katika biashara ya utumwa zimekuwa miongoni mwa turathi muhimu za historia ya Marekani, historia ya kushinda, ushindi na Uhuru.
Aliongezea: "Marekani iliwapatia mafunzo na kuwapeleka mashujaa wetu katika maeneo hayo ,na kufanikiwa kushinda vita viwili vya duniani. Hivyobasi utawala wangu hautafikiria kubadilisha majina ya kambi hizi na hata vifaa vya kijeshi.Historia yetu kama taifa lenye uwezo mkubwa duniani haitaingiliwa, Heshimuni jeshi letu.
Afisa anayesimamia masuala ya habari katika Ikulu ya Whitehouse Kayleigh McEnany alisema katika taarifa kwa vyombo vya habari baadaye kwamba uwezekano wa kubadilisha majina ya kambi hizo za kijeshi , haupo kwa rais Trump.
Alisema kwamba hatotia saini sheria yoyote ambayo itapitishwa na bunge la Congress inayohitaji majina hayo kubadilishwa.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment