Search This Blog
Saturday, June 6, 2020
Serikali yaandaa mfumo wa Kielektroniki Uhakiki madeni hewa
Serikali inaandaa mfumo wa kielektroniki, utakaotumika katika kukusanya na kulipa madeni yote ya watumishi wa umma, ili kuondokana na tatizo la udanganyifu kunakosababisha kuwepo kwa madeni hewa.
Mpango huo wa serikali umetangazwa jijini Dodoma na Rais Dkt. John Magufuli, wakati alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Nchini (CWT), unaoambatana na uchaguzi mkuu wa viongozi wa chama hicho, na kusisitiza serikali inaendelea kulipa madeni ya watumishi wake wakiwemo walimu, lakini ni baada ya kuyahikiki madeni hayo.
Pamoja na mambo mengine, Rais akachukua wasaa huo kuwahimiza watanzania kwa mara nyingine tena, kuacha kupokea misaada ya barakoa wasizozijua zinatoka wapi, huku akiwakumbusha viongozi wa ngazi mbalimbali wajibu wao wa kuwalinda wananchi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment