Search This Blog
Monday, June 22, 2020
Saudi Arabia yapiga marufuku raia kutoka mataifa mengine kufanya ibada ya Hija
Saudi Arabia imepiga maarufuku raia kutoka mataifa mengine kufanya ibada ya Hija nchini humo mwaka huu ili kudhibiti virusi vya corona.
Ni idadi ndogo tu ya watu wanaoishi kwa sasa katika ufalme huo watakaoweza kushiriki Hija, kulingana na tangazo lililotolewa kwenye vyombo vya habari vya taifa hilo.
Watu takriban milioni mbili vinginevyo wangetembelea Maka na Madina msimu wa kiangazi kwa ajili ya Hija hiyo inayofanyika kila mwaka kulingana na imani ya kiislamu.
Kumekuwa na hofu kwamba Hija inaweza kufutwa kabisa.
Kwa kawaida Hija ni moja ya vipindi muhimu katika kalenda ya dini ya Kiislamu.Lakini ni raia kutoka nchi nyingine ambao tayari ni wakazi wa Saudi Arabia watakaoruhusiwa kuhudhuria Hija ya mwaka huu.
Waumini wakisali kwa kuzingatia amri ya kutokaribiana mjini Mecca mwezi Aprili
Maafisa nchini humo wanasema hii ndio njia pekee itakayowezesha kufanya mipango ya kutokaribiana ambayo itawezesha watu wawe salama.
Saudi Arabia imerekodi visa vya corona 161,005 na vifo vilivyotokana na ugonjwa huo ni 1,307.
Hija ni mojawapo ya nguzo tano za Kiislamu ambayo kila Muislamu hutakiwa kuitekeleza walau mara moja.
Kila Muislamu, mwenye afya nzuri na aliye na uwezo anapaswa kutimiza nguzo hii ili kuishi maisha mazuri na ya uwajibikaji, kwa mujibu wa dini ya Kiislamu.
Mahujaji hukusanyika mjini Mecca kusimama mbele ya Kaaba, wakimsifu Allah (Mola) Mungu pamoja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment