Search This Blog
Monday, June 15, 2020
Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson atangaza kugombea ubunge
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge, katika jimbo ambalo hakulitaja na kusema kuwa muda ukifika atatoa taarifa ya wapi ataenda kugombea.
Dkt. Tulia ameyasema hayo bungeni mjini Dodoma katika mkutano wa 19, kikao cha 46 alipopewa nafasi ya kuzungumza ambapo pamoja na kuweka wazi kusudio la kugombea, pia ameipongeza serikali kwa hatua mbalimbali ilizochukua kuhakikisha inawaletea wananchi maendeleo.
“Nami nimepata hamasa ya kujitosa. Na Inshallah Mwenyenzi Mungu atujalie uzima na afya, yumkini nitakwenda mahali fulani, kuomba ridhaa ya wananchi wenzangu ya kuwatumikia katika bunge lako [Spika wa Bunge] tukufu,” amesema Tulia.
Aidha, kiongozi huyo hajaweka wazi atagombea jimbo gani, lakini kumekuwapo tetesi kuwa huenda akagombea katika Jimbo la Mbeya Mjini ambalo sasa linaongozwa na Mbunge Joseph Mbilinyi kupitia CHADEMA.
Novemba 2015 baada ya kuingia madarakani, Rais Dkt. Magufuli alimteua Dkt. Tulia kuwa mbunge ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment