Search This Blog
Monday, June 1, 2020
Museveni aahirisha mpango wa kufungua taasisi za elimu
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuwa Shule, makanisa, misikiti, vilabu, vilabu vya usiku, maeneo ya kufanyia mazoezi na saluni za urembo zitaendelea kufungwa ili kuepuka maambukizi ya virusi vya corona.
Museveni amesema kuwa si rahisi kwa maeneo hayo kufuata masharti ya kutochangamana.
Amri ya kutotembea usiku
Rais Museveni pia amesema muda wa kuwa ndani ya nyumba utaendelea kuwa kuanzia saa moja usiku mpaka saa kumi na mbili kamili asubuhi kwa siku 21 zaidi.
Makanisa, vilabu vya pombe, vilabu vya usiku , maeneo ya kufanya mazoezi na sauna yataendelea kufungwa kwa siku 21, huku kufungua shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kukiwa kumeahirishwa wakisubiri kwa mwezi mmoja.
''Tumeamua kuahirisha kufunguliwa kwa shule kwa wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mitihani kwa mwezi mmoja zaidi tukijiandaa zaidi na kutazama hali ilivyo''.Alisema
Wenye magari ya dalala wamemaliza miezi miwili na nusu bila kazi tangu marufuku ilipowekwa mwezi Machi.
'Kuanzia tarehe nne nitaruhusu kuanza tena kwa usafiri wa Umma wa mabasi , usafiri wa abiria wa treni na dalala kuchukua abiria idadi ya nusu''. Alisema Rais Museveni.
Viwanja vya ndege vitaendelea kufungwa pia magari binafsi hayataruhusiwa kufanya kazi katika maeneo ya mpakani
Viongozi wa dini mwishoni mwa Juma lililopita waliomba nyumba za ibada baada ya kuchukua hatua ya kufungua masoko , kilio ambacho hakijasikilizwa na kiongozi huyo akiwataka waumini waendelee kusali kwa njia za televisheni wakiwa katika nyumba zao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment