Search This Blog
Wednesday, June 10, 2020
"Kujiepushe na mifarakano na kushambuliana, hatua ya kwanza ya kujenga Umoja wa Kiislamu"
Katibu Mkuu wa Baraza la Kimataifa la Kukurubisha Pamoja Madhehebu Mbalimbali ya Kiislamu amesema kuwa, jengo la umoja na mshikamano baina ya Waislamu linahitajia kuchukuliwa hatua kadhaa za utangulizi ambapo hatua ya kwanza kabisa muhimu ni kujiweka mbali na mifarakano na kuacha kushambuliana mataifa ya Waislamu.
Sheikh Hamid Hawali Shahriari alisema hayo jana Jumatano hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, nchi za Kiislamu zinaweza kuwa na umoja na mshikamano madhubuti na hivyo kuupa nguvu kubwa ulimwengu wa Kiislamu.
Aidha amesema, maadui wanafanya njama nyingi za kila namna za kuhakikisha kuwa Waislamu hawawi kitu kimoja ndio maana huwa mara kwa mara wanaanzisha makundi mbalimbali ya kuwagombanisha Waislamu na kujenga uadui na chuki katika safu za Waislamu.
Ametoa mifano ya makundi hayo kuwa ni yale ya Mashia wa serikali ya Uingereza na Masuni wa serikali ya Marekani na magenge ya kigaidi kama Daesh (ISIS) yaliyoanzishwa na maadui wa Uislamu ili kuzusha moto wa vita katika ulimwengu wa Kiislamu na kuzivamia na kuzipora nchi za Waislamu utajiri wao.
Sheikh Shahriari vile vile amesisitiza kuwa, hatua ya pili ya kurahisisha kupatikana umoja na mshikamano katika ulimwengu wa Kiislamu ni ushirikiano katika kukabiliana na maadui na kusaidiana Waislamu wakati wanapovamiwa na maadui.
Katibu Mkuu huyo wa Baraza la Kimataifa la Kukurubisha Pamoja Madhehebu Mbalimbali ya Kiislamu aidha amesema, hatua ya tatu ya kuleta umoja na mshikamano kati ya Waislamu ni kufanya kazi kwa pamoja kwa namna ambayo Waislamu washirikiane katika nguvu zao zote za kiuchumi, kisiasa, kiusalama na kielimu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment