Search This Blog
Thursday, June 4, 2020
IGP Sirro Atoa Maelekezo kwa Wakuu wa Polisi wa Wilaya
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewaagiza Wakuu wa Polisi wa Wilaya OCDs kuhakikisha wanasimamia mikutano wakati wa kampeni ili iwe ya amani na utulivu.
IGP Sirro amesema hayo leo akiwa mkoani Simiyu wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika mkoa huo na kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo ambapo alisema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga kusimamia uchaguzi na kwamba litaendelea kutoa elimu kwa wananchi ikiwa pamoja na kushirikiana ipasavyo na wadau wa uchaguzi.
Aidha, IGP Sirro amewapandisha vyeo askari wawili wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia FFU mkoa wa Simiyu kutoa cheo cha konstebo wa Polisi na kuwa Koplo wa Polisi kutokana na umahili wao wa kutekeleza majukumu wanayopewa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment