Search This Blog

Wednesday, June 24, 2020

Askari 7 wauawa katika shambulizi Afghanistan


Askari 7 wameuawa katika shambulizi la silaha lililotekelezwa na wanamgambo wa Taliban katika kituo cha jeshi magharibi mwa Afghanistan.

Wizara ya Ulinzi imetangaza kwamba wanamgambo walishambulia kituo cha jeshi katika kijiji cha Akazi wilayani Bala Murgab.

Imeelezwa kuwa askari 7 wamepoteza maisha yao na askari 5 wamejeruhiwa katika shambulizi hilo.

Hata hivyo, inasemekana kuwa Taliban nao wamepoteza idadi kubwa ya wanamgambo wao wakati wa shambulizi hilo.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...