Search This Blog
Monday, June 1, 2020
Asilimia 42 ya wanachuo wamewasili na kuanza masomo UDOM
Idadi ya wanafunzi 12,000 sawa na asilimia 42 wamewasili na kuanza masomo katika chuo kikuu cha Dodoma UDOM ikiwa ni siku ya kwanza ya kuanza kwa masomo baada ya likizo ya Zaidi ya miezi miwili kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM Prof. Faustine Bee ameeleza kuwa pamoja na idadi hiyo kuwa chini masomo yameanza hii leo nakutoa wito kwa ambao bado hawajawasili chuoni waharakishe ili kuhitimisha muhula kwa pamoja.
Pia Prof. Bee amewatoa hofu wanafunzi kuwa muhula huu wa masomo utamalizika kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kushiriki katika uchaguzi huo kama ambavyo imekuwa ikifanyika miaka yote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment