Search This Blog

Tuesday, June 2, 2020

Alikiba atimiza ahadi kwa mashabiki zake

Staa wa muziki ndani na nje ya Tanzania Alikiba, ametimiza ahadi yake aliyowaahidi mashabiki wake ya kwamba, ataachia kazi mpya mara baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuisha.


Hilo limejidhirisha kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, baada ya kutangaza kuachia kazi mpya iitwayo "so hot".

"Tuna makubaliano mazuri kwenye uongozi na mimi ndiyo C.E.O, lazima watu wawe na muamko mzuri kwa sababu watu wamenimiss, nawaambia mashabiki zangu kwamba mwezi wa Ramadhan ukiisha, kuna ngoma ya ajabu sana inakuja, nawaambia ukweli maana sijawahi kusema hivi" amesema Alikiba.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...