UONGOZI wa Simba umesema kuwa mechi yao ya Kombe la Shrikisho hatua ya robo fainali dhidi ya Azam FC itakuwa ni ngumu na ya kisasi.
Jana, ratiba ya hatua ya robo fainali ilipangwa ambapo Simba itakutana na Azam FC ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo walilolitwaa kwa kuitwanga Lipuli FC bao 1-0.
Sven Vandernbroeck, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa anaamini utakuwa mchezo mgumu kutokana na Azam FC kuwa ni mabingwa watetezi na waliwafunga walipokutana kwenye mechi ya ligi.
"Utakuwa ni mchezo mgumu ukizingatia kwamba Azam FC tuliwafunga kwenye mechi yetu tulipokutana hivyo watajipanga kulipa kisasi.
"Tunajiandaa vizuri ili kuona namna gani tutapata matokeo kwani kila mechi kwetu tunachotazama ni matokeo," amesema.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Juni 27 Uwanja wa Taifa, mshindi wa mchezo huo atakutana na mshindi kati ya Yanga ama Kagera Sugar.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment