Search This Blog

Sunday, May 17, 2020

Polisi Simiyu yamnasa aliyebaka mtoto wa miaka mitano


Jeshi la Polisi Mkoani Simiyu, linamshikilia Mkazi wa Wilaya ya Bariadi, Ndamo Mabula (25) kwa tuhuma za kumbaka Mtoto mdogo wa miaka mitano (5) baada ya kumvizia mtoto huyo wakati wazazi wake wamekwenda shambani na kisha kutekeleza kitendo hicho cha kikatili na kwamba Jeshi hilo linatarajia kumfikisha Mahakamani wakati wowote kuanzia sasa Kijana huyo.

Baada ya kijana huyo kufanya kitendo hicho alikimbia huku mtoto huyo akipiga kelele za kuomba msaada na ndipo Wananchi walipojitokeza kumsaidia na alipoulizwa aliweza kumtaja kijana huyo na hivyo Wananchi wakaanza kumtafuta na kufanikiwa kumkamata na kisha kumfikisha Polisi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...